WANAOHAMSISHA KUSUSIA UCHAGUZI WAULIZENI FAMILIA ZAO ZIKO WAPI? OSCAR EDGAR EMBEDODO

Mkazi wa Manispaa ya Sumbawanga, Mkoa wa Rukwa, Oscar Edgar Embedodo, ametahadharisha wananchi wa Sumbawanga na Watanzania kwa ujumla juu ya hatari ya kushawishiwa kususia uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025.

Amesema kuwa ushawishi huo si wa kawaida, bali ni kiashiria cha mpango wa kuvuruga amani ya nchi kwa maslahi binafsi ya kisiasa.

Embedodo ameonya kuwa baadhi ya watu wenye nia ovu tayari wameanza kuhamisha familia zao na kuzipeleka katika nchi zinazowafadhili kuleta vurugu ndani ya Tanzania. Amehoji kuwa kama kweli watu hao wanamaanisha amani na ustawi wa taifa, kwa nini familia zao hazipo nchini kushuhudia matokeo ya kile wanachohubiri?

Ametoa wito kwa Watanzania kuwa makini, kuwahoji na kutowafuata viongozi wa namna hiyo. Amewahimiza wajitayarishe kushiriki kikamilifu katika uchaguzi kwa amani, kwa kuwa uchaguzi ni haki ya msingi ya kila raia na njia ya kujenga taifa lenye maendeleo na mshikamano wa kweli.

#MSLAC #Katibanasheria #Hakingowi #SisiTanzania #Katibanasheria

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *