UCHAGUZI NI HAKI YA KIKATIBA, SIYO KWA MAELEKEZO YA MAKU

Mzee Shila Hailele Mponda, mkazi wa Jimbo la Tunduma, ameibua hoja nzito dhidi ya kampeni ya “No Reforms No Election” inayoendeshwa na kikundi cha Mwenyekiti wa chama hicho, Tundu Lissu.

Mzee Shila ameeleza kuwa tayari wanasiasa wa CHADEMA kutoka jimbo lao, akiwemo aliyekuwa Mbunge Frank Mwakajoka na mwanasiasa kijana Boniface Mwakabanje, wameshatangaza nia ya kugombea ubunge.

Amesema kuwa kikundi cha Tundu Lissu kinachopinga uchaguzi hakina mvuto wala uungwaji mkono katika Jimbo la Tunduma, kwani wananchi wanaelewa kuwa uchaguzi ni haki ya kikatiba.

Kwa mujibu wa Mzee Shila, hakuna mtu au kikundi kinachopaswa kuzuia raia yeyote kugombea ifikapo mwezi Oktoba, kama katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inavyoelekeza.

Kwa msingi huo, Mzee Shila amemuomba Rais Samia Suluhu Hassan kuhakikisha uchaguzi mkuu haucheleweshwi wala kusitishwa kwa sababu ya shinikizo au kelele za kisiasa kutoka kwa kundi lolote, bali uendelee kama ilivyopangwa kikatiba.

#sisinitanzania #MSLAC #Katibanasheria #Tanzania

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *