ZANZIBAR

Mkurugenzi wa Ofisi ya Zanzibar ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Adam Mkina leo tarehe 24 Februari, 2026, ametembelea mafunzo kwa Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi wa vituo vya kupigia kura katika Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Mkoani Songwe ambapo amewataka watendaji hao kufanya kazi kwa weledi

Mkina amewaasa washiriki wazingatie mafunzo waliyoyapata na kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria za uchaguzi ili kufanikisha uchaguzi huo. Amewasisitiza kuzingatia viapo walivyoapa, kuzingatia ujazaji wa fomu za uchaguzi katika hatua zote za uchaguzi ili kuepuka changamoto zinazoweza kujitokeza na kwamba inapotokea changamoto katika vituo washirikiane kuzitatua ili …

Soma zaidi »

Naibu Waziri Ofisi Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Festo Dugange amefanya mazungumzo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais (Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi ) Mhe.Hamza Hassan Juma wakati wa ziara ya kikazi leo Februari 16, 2026 Zanzibar.

Katika mazungumzo yao viongozi hao wamesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa Serikali hizo mbili katika kulinda Muungano. Naibu Waziri Dkt. Dugange alipongeza kazi kubwa ya maendeleo inayofanywa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) chini ya Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi. Alisema kuwa kupitia maendeleo hayo yanaimarisha uchumi wa Zanzibar na …

Soma zaidi »

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akipanda mti wa Muembe (Mangifera indica) katika eneo la Bungi Kilimo, Mkoa wa Kusini Unguja tarehe 27 Januari, 2026, wakati wa kumbukumbu ya siku yake ya kuzaliwa. Rais Mhe. Dkt. Samia alizaliwa tarehe 27 Januari, 1960 katika Kijiji cha Kizimkazi, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar

Soma zaidi »

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akivuta kitambaa pamoja na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Rais Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete kama ishara ya uzinduzi wa Jengo la Taaluma na Utawala na Bweni la Wanafunzi la Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Taasisi ya Sayansi za Bahari, Buyu Zanziba

Soma zaidi »