Waziri Mkuu

🔴#LIVE: WAZIRI MKUU ANAZUNGUMZA NA WAMACHINGA, MADEREVA PIKIPIKI NA BAJAJI

Waziri Mkuu anazungumza moja kwa moja na wamachinga, madereva wa pikipiki na bajaji kuhusu masuala yanayowagusa katika shughuli zao za kila siku. Katika mazungumzo haya, anasikiliza changamoto zao, anatoa maelekezo, na kufafanua msimamo wa serikali katika kuboresha mazingira ya kazi na maisha ya wananchi wa kipato cha chini. Video hii …

Soma zaidi »

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kabla ya kuzungumza na Wazee wa Mkoa wa Dar es Salaam katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam tarehe 02 Desemba, 2025.

Soma zaidi »

DKT. MWIGULU AKUTANA NA KATIBU MKUU WA TEC

Waziri Mkuu, Mhe. Dkt. Mwigulu Nchemba, leo Novemba 20, 2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Padri Charles Kitima, katika Ofisi Ndogo ya Waziri Mkuu, Magogoni jijini Dar es Salaam.

Soma zaidi »

RAIS SAMIA AZUNGUMZA MARA BAADA YA KUAPISHA MAWAZIRI NA NAIBU MAWAZIRI

Leo, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ametoa hotuba muhimu mara baada ya kuwaapisha Mawaziri na Naibu Mawaziri wapya Ikulu. #RaisSamia #MawaziriWapya #Ikulu #HotubaYaRais #Tanzania

Soma zaidi »

WAZIRI MKUU DKT. MWIGULU NCHEMBA AMEKABIDHIWA RASMI OFISI NA WAZIRI MKUU MSTAAFU KASSIM MAJALIWA

Waziri Mkuu Dkt. Mwigulu Nchemba alikabidhiwa rasmi ofisi na Waziri Mkuu Mstaafu Kassim Majaliwa Novemba 17, 2025, Mlimwa, Dodoma. Hafla ilihudhuriwa na viongozi mbalimbali ikiwa ni pamoja na Naibu Waziri Mkuu Mstaafu Dkt. Doto Biteko, Makatibu Wakuu, Wakuu wa Taasisi na watumishi wa Ofisi ya Waziri Mkuu.

Soma zaidi »

DKT. MWIGULU AAPISHWA IKULU CHAMWINO—RAIS SAMIA AELEZA SABABU ZA UTEUZI WAKE

Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amemuapisha Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Katika hotuba yake, Rais Samia amesema uteuzi huo ulipitia ushindani mkubwa na Dkt. Mwigulu ndiye aliyebeba sifa nyingi zaidi kwenye vigezo vyote vilivyopimwa. Ameeleza kuwa majukumu ya Waziri Mkuu …

Soma zaidi »

RAIS DKT. SAMIA AKIMUAPISHA MWIGULU NCHEMBA KUWA WAZIRI MKUU WA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimuapisha Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania katika hafla inayofanyika Ikulu Chamwino, Dodoma, tarehe 14 Novemba, 2025.

Soma zaidi »

BREAKING NEWS: MWIGULU NCHEMBA ATANGAZWA WAZIRI MKUU LEO BUNGENI 🇹🇿

Leo bungeni, Spika ametangaza rasmi uteuzi wa Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tangazo hilo limepokelewa kwa shangwe na pongezi kutoka kwa wabunge na wananchi nchini kote. Tazama video hii kwa taarifa kamili kutoka Bungeni Dodoma na maoni ya viongozi mbalimbali. #Tanzania #MwiguluNchemba #WaziriMkuu …

Soma zaidi »

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anatambua kwa dhati mchango wa madhehebu ya dini ikiwemo BAKWATA na wadau wote wa elimu katika kuimarisha maadili, kuendeleza maarifa na kuleta mshikamano wa kitaifa kupitia elimu.

Amesema kuwa elimu haiwezi kukamilika kama hakuna maadili kwani ndiyo yanayojenga utu, heshima na mshikamano wa kijamii. “Serikali ya Awamu ya Sita imekuwa mstari wa mbele kuhakikisha elimu inakuza maarifa na ujuzi, sambamba na malezi yanayoimarisha tabia bora na maadili ya kizalendo kwa vijana wa Kitanzania”. Amesema hayo Jumamosi Septemba …

Soma zaidi »

Maonesho ya Nane ya Kitaifa ya Teknolojia ya Madini Geita yanatarajiwa kuzinduliwa kesho na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa katika Viwanja vya Dkt. Samia Suluhu Hassan, Bombambili, Manispaa ya Geita.

Akizungumza leo, Afisa Madini Mkazi wa Mkoa wa Geita, Samwel Shoo, amesema Tume ya Madini inashiriki maonesho hayo kwa mara ya nane mfululizo na imeandaa huduma za elimu kwa wadau wote wa sekta ya madini watakaotembelea mabanda yake. Elimu hiyo itahusu teknolojia za kisasa za utafiti, uchimbaji na uchenjuaji wa …

Soma zaidi »