Daraja la Kigongo–Busisi, maarufu kama Daraja la John Pombe Magufuli, ni mradi mkubwa wa miundombinu unaounganisha Mkoa wa Mwanza na Geita, Tanzania. Kwa urefu wa kilomita 3.2, daraja hili litakuwa daraja refu zaidi Afrika Mashariki na la sita kwa urefu barani Afrika 🌍.
Kabla ya ujenzi wa daraja hili, safari kati ya Kigongo na Busisi ilihitaji kivuko kwa muda wa dakika 35 hadi saa 3, lakini sasa, kwa kukamilika kwa daraja hili, safari hiyo itachukua dakika 5 pekee! 🚗⏳
Mradi huu unaogharimu $308.88 milioni umetekelezwa na Serikali ya Tanzania kwa kushirikiana na kampuni za ujenzi kutoka China (CCECC & CR15B). Kufikia Januari 2025, ujenzi umefikia asilimia 96.3, na daraja linatarajiwa kukamilika mwishoni mwa Februari 2025.
📊 Takwimu Muhimu:
✅ Gharama: TZS bilioni 611
✅ Ajira zilizotolewa: 29,211 (93.33% Watanzania)
✅ Magari yatakayopita kila siku: 10,200
✅ Njia za magari: Mita 7 kila moja
✅ Njia za dharura: Mita 2.5 kila upande
✅ Njia za watembea kwa miguu: Mita 2.5 kila upande Daraja hili ni ushuhuda wa maendeleo makubwa chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, likichochea biashara, usafiri na uchumi wa Kanda ya Ziwa, na hata nchi jirani kama Uganda, Rwanda na Burundi. 🌍💼🚛
Usisahau ku-LIKE, KUSHARE, na KUSUBSCRIBE kwa maudhui zaidi ya maendeleo ya Tanzania! 🇹🇿💙
#KigongoBusisiBridge #MaendeleoTanzania #SamiaSuluhuHassan #TanzaniaKwaMaendeleo
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+