Arusha, Machi 1, 2025 – Meya wa Jiji la Arusha, Mhe. Maximilian, ametangaza kuwa zaidi ya watu laki nne wanatarajiwa kushiriki katika kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yatakayofanyika jijini Arusha.
Akizungumza na waandishi wa habari leo, Mhe. Maximilian amesema maandalizi yanaendelea vizuri, huku jiji likijiandaa kupokea wageni kutoka ndani na nje ya Tanzania. “Maadhimisho haya ni fursa muhimu ya kutambua mchango wa wanawake katika maendeleo ya taifa letu. Tumeshuhudia jitihada za wanawake katika sekta mbalimbali, na siku hii ni ya kusherehekea mafanikio yao,” alisema.
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+