
Mhe. Dkt. Biteko alisema kuwa Sekta ya Ununuzi na Ugavi ndio eneo pekee linalochukua takribani asilimia 70 ya Bajeti ya Serikali, hivyo uadilifu pekee ndio utakaosaidia fedha kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa hasa katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.
Mhe. Dkt. Biteko alisema kuwa Sekta ya Ununuzi na Ugavi ndio eneo pekee linalochukua takribani asilimia 70 ya Bajeti ya Serikali, hivyo uadilifu pekee ndio utakaosaidia fedha kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa hasa katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Aidha, Dkt. Biteko aliwaasa Wataalamu hao kuzingatia na kuyaishi yale yaliyopo kwenye sheria za manunuzi kwa kufanya kazi yenye tija, uwazi na kujiepusha na vitendo vya rushwa kwenye masuala yote ya manunuzi ya Umma.
‘’Serikali iliamua kuanzisha sheria ya manunuzi ili kuwa na manunuzi yenye tija, kupata bidhaa zenye ubora na wakati, na kuondoa mianya ya rushwa., hivyo naomba mkutano huu uzingatie yale yanayotafsiriwa kwenye sheria hiyo’’alisema Mhe. Dkt. Biteko.
Mhe Biteko aliipongeza Bodi ya Usimamizi wa Ununuzi na Ugavi (PSPTB), kwa hatua mbalimbali inazochukua hasa kwa wale wanaoenda kinyume na maadili ya sekta hiyo na kusisitiza kuwa Serikali kupitia bodi hiyo haitasita kuwachukulia hatua kali watumishi ambao watashindwa kutekeleza majukumu yao kwa kuzingatia sheria zilizopo.
Awali akimkaribisha Naibu Waziri Mkuu, Naibu Waziri wa Fedha, Mhe. Hamad Hassan Chande (Mb), alisema kuwa Wizara ya Fedha imeendelea kuwapa thamani na kutoa kipaumbele kwa wataalamu wa ununuzi na ugavi ili kuhakikisha wanafanya vizuri katika eneo lao la kazi ili kukuza uchumi.
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+