Maktaba ya Mwezi: January 2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-Organ) Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC katika ukumbi wa New Parliament Building, Harare nchini Zimbabwe tarehe 31 Januari, 2025

Mkutano huo pamoja na mambo mengine unajadili hali ya ulinzi na usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).

Soma zaidi »

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-Organ) Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Asasi hiyo uliofanyika Ikulu Jijini Dar es Salaam tarehe 28 Januari, 2025

Katika Mkutano huo, Mhe. Rais Dkt. Samia alishiriki pamoja na Rais wa Jamhuri ya Zambia Mhe. Hakainde Hichilema sambamba na Rais wa Jamhuri ya Malawi Mhe. Dkt. Lazarus McCarthy Chakwera. Aidha, Rais wa Jamhuri ya Afrika Kusini Mhe. Cyril Ramaphosa na Rais wa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC) Mhe. …

Soma zaidi »

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akikagua mabanda ya maonesho ya wadau wa sekta ya maji nje ya Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City mkoani Dar es Salaam kabla ya kufungua Kongamano la Nne la Kimataifa la Kisayansi la Maji linalofanyika kwa siku tatu kuanzia Jumatano Januari 29, 2025 mpaka Ijumaa Januari 31, 2025

Soma zaidi »

MELEFU WAJITOKEZA KUPATA ELIMU NA MSAADA WA KISHERIA UZINDUZI MSLAC MKOA WA 17 WA KILIMANJARO TAREHE 29/1/2025

Kampeni ya Samia Legal Aid Campaign (MSLAC) imepiga hatua kubwa tangu ilipoanzishwa, na uzinduzi wa mkoa wa 17 Kilimanjaro mnamo 29 Januari 2025 ni uthibitisho wa mafanikio yake katika kuenea kitaifa. Hapa ni tathmini ya maendeleo ya kampeni hii tangu kuanzishwa kwake: 1. Ufanisi wa Kampeni Hadi Sasa – MSLAC …

Soma zaidi »

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akifanya Mazungumzo na NaibuMkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Bw. Bo Li

Mazungumzo hayo yalifanyika kando ya Mkutano waNishati wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika unaofanyikakatika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC)

Soma zaidi »

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Benki ya Uwekezaji wa Miundombinu (Asian Infrastructure Investment Bank – AIIB), Bw. Jin Luqun

Wamekutana na kuzungumza kando ya Mkutano wa Nishati wa Wakuu wa nchi na Serikali wa Afrika, ulioanza (27.01.2025), katika Kituo cha Kimataifa cha Mikutano Cha Julius Nyerere (JNICC), Jijini Dar es Salaam, ambapo pamoja na mambo mengine, walijadiliana namna ya kuendeleza ushirikiano wa katika kuboresha miundombinu nchini, ukiwemo Mradi wa …

Soma zaidi »