“LEO DISEMBA 31, 2024 MWISHO MATUMIZI YA KUNI NA MKAA KWA TAASISI ZA UMMA”- MAJALIWA.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Kassim Majaliwa Majaliwa amezikumbusha Taasisi na mashirika yote ya Serikali yaliyopo kote nchini Tanzania ambayo yanahudumia watu zaidi ya 100, kutekeleza bila shuruti agizo lake la kuitangaza Disemba 31, 2024 kuwa siku ya mwisho kwa matumizi ya Mkaa na Kuni kwenye shughuli za Mapishi.

Waziri Mkuu Mhe. Majaliwa ametoa kauli hiyo mapema Leo Jumanne Disemba 31, 2024 wakati akihutubia wananchi kwenye Tamasha la Azimio la Kizimkazi 2024, linalofanyika kwa mara ya pili Ruangwa Mkoani Lindi ikiwa ni mara baada ya kuzinduliwa kwake mapema mwaka huu na Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Kizimkazi Visiwani Zanzibar.

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *