Wana-Dodoma na Watanzania kwa ujumla, mnakaribishwa kushiriki katika Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Kupiga Vita Matumizi na Biashara ya Dawa za Kulevya kitakachofanyika tarehe 26 Juni 2025, kuanzia saa 1:00 asubuhi, katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete Convention Centre, Dodoma.
Mgeni rasmi atakuwa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Tukio hili litatumika kutoa elimu juu ya madhara ya dawa za kulevya kwa jamii na taifa. Jitokeze kwa wingi – Tuijenge Tanzania isiyo na dawa za kulevya!
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+