VIJANA WALIOACHANA NA DAWA ZA KULEVYA WAIPONGEZA DCEA

Baadhi ya vijana waliowahi kuwa watumiaji wa dawa za kulevya wameipongeza Mamlaka ya Kudhibiti na Kupambana na Dawa za Kulevya (DCEA) kwa juhudi zake thabiti katika kupambana na biashara na matumizi ya dawa hizo. Vijana hao Pendo Athuman, Tonny Michael na Gabriel Nyangasi wamesema kuwa hatua zilizochukuliwa na mamlaka hiyo, ikiwemo kuziba mianya ya usafirishaji na usambazaji wa dawa za kulevya, zimechangia kwa kiasi kikubwa kupungua kwa upatikanaji wa dawa hizo mitaani, jambo ambalo limekuwa msaada mkubwa kwao na kwa wengine walioko katika safari ya kuachana na uraibu huo.

Wameeleza kuwa kwa sasa DCEA haijajikita tu katika ukamataji, bali pia inawekeza kikamilifu katika kutoa elimu ya kinga pamoja na huduma za tiba kwa waathirika wa dawa za kulevya, jambo walilolieleza kuwa ni la kupongezwa kwani linagusa maisha ya moja kwa moja ya vijana wengi waliokuwa hatarini.

Aidha, wamepongeza juhudi za Serikali chini ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania pamoja na Mahakama kwa kusimamia sheria na kutoa hukumu stahiki kwa wote wanaobainika kushiriki katika biashara ya dawa za kulevya, wakisema hatua hizo zinaongeza hofu kwa wahusika na kulinda kizazi cha sasa na baadaye.

Kauli mbiu: “Wekeza kwenye Kinga na Tiba dhidi ya dawa za kulevya”

#DCEA #OktobaTunatiki

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *