RAIS SAMIA AZUNGUMZA NA WANANCHI BAADA YA KUFUNGUA DARAJA LA JP MAGUFULI (KIGONGO–BUSISI)

Mwanza, 19 Juni 2025 – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amezungumza na wananchi katika viwanja vya Chuo cha Ufundi Kalwande, jijini Mwanza, mara baada ya kuzindua rasmi Daraja la JP Magufuli (Kigongo–Busisi) lenye urefu wa kilomita 3.0.

Katika hotuba yake, Rais Samia amepongeza juhudi za watanzania na wataalamu wa ndani kwa kukamilisha mradi huo mkubwa wa kimkakati, akisisitiza kuwa daraja hilo ni alama ya uendelezaji wa ndoto ya Hayati Dkt. John Magufuli na ishara ya kasi ya maendeleo inayoendelea chini ya Serikali ya Awamu ya Sita.

Unaweza kuangalia pia

🔴 LIVE: SAMIA SULUHU HASSAN AINGIA KWA KISHINDO MBEYA – MBALIZI

Rais Samia Suluhu Hassan amewasili Mbalizi, Mbeya, kwa kishindo kikubwa akipokelewa na umati wa wananchi …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *