Mkoani Mwanza – Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, leo anazindua rasmi Daraja la Kigongo–Busisi, mradi mkubwa uliokuwa ndoto ya Hayati Dkt. John Pombe Magufuli.
Daraja hilo, ambalo ujenzi wake ulianza rasmi chini ya utawala wa Magufuli, limekamilika kikamilifu chini ya uongozi wa Rais Samia, likiwa na urefu wa kilomita 3.2 na kuunganisha mikoa ya Mwanza na Geita bila kutumia kivuko.
Rais Samia amesema uzinduzi huu ni ishara ya kutimiza ndoto za maendeleo na kuendeleza maono ya watangulizi wake kwa vitendo, huku akisisitiza kuwa serikali yake itaendelea kutekeleza miradi mikubwa kwa manufaa ya Watanzania wote.
✨ Usisahau kusubscribe, kupenda na kushiriki video hii ili kuungana na safari ya maendeleo ya Tanzania!
#DarajaKigongoBusisi #MagufuliLegacy #RaisSamia #MaendeleoTanzania #KandaYaZiwa #TanzaniaInajengwa
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+