Katika kutambua mchango mkubwa wa Rais wa Benki ya Maendeleo ya Afrika katika utekelezaji wa miradi hiyo na katika kuchangia maendeleo ya miundombinu nchini Tanzania, Rais Dkt. Samia ameridhia pendekezo la Wizara ya Ujenzi la kuipa jina barabara hiyo ya mzunguko wa nje wa Dodoma la “Barabara ya Dkt. Akinwumi Adesina.
” Akiwa nchini, Dkt. Adesina alitunukiwa Shahada ya Heshima ya Udaktari wa Sayansi (Honoris Causa) na Chuo Kikuu cha Dar es Salaam kutokana na mchango wake mkubwa kwa maendeleo ya Bara la Afrika kupitia sera za fedha na programu bunifu za maendeleo.
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+