Recent Posts

Ushirikiano wa Wananchi na Serikali katika Kuboresha Huduma za Afya

Kituo cha Afya Kafita, kilichopo katika Wilaya ya Nyang’hwale, Kata ya Kafita, kijiji cha Kafita, ni mfano wa mafanikio ya ushirikiano kati ya wananchi, Mfuko wa Maendeleo ya Jamii (TASAF), na serikali kuu. Ujenzi wa kituo hiki umegharimu jumla ya shilingi milioni 200, fedha ambazo zilitokana na juhudi za wananchi, …

Soma zaidi »

Shule ya Sekondari ya Geita Girls imekuwa miongoni mwa miradi muhimu ya serikali inayolenga kuboresha sekta ya elimu nchini Tanzania. Hadi sasa, ujenzi wa shule hii umegharimu takribani TZS bilioni 4.35. Shule hii imeanza kupokea wanafunzi, na tayari zaidi ya wanafunzi 100 wapo shuleni hapo wakijifunza katika mazingira bora na ya kisasa

Licha ya mafanikio haya, juhudi za ujenzi bado zinaendelea. Mabweni ya kisasa yamepangwa kujengwa ili kuhakikisha wanafunzi wanapata sehemu salama za kuishi, na ukumbi wa mikutano unaendelea kujengwa kwa lengo la kuwapa wanafunzi na walimu nafasi ya kushiriki mikutano na shughuli mbalimbali za kitaaluma na kijamii. Kuimarisha Usawa wa Kijinsia …

Soma zaidi »

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Kassim Majaliwa, ameweka jiwe la msingi katika ujenzi wa Daraja la Sukuma lenye urefu wa mita 70 pamoja na barabara unganishi yenye urefu wa kilomita 2.3

Hafla hiyo ilifanyika katika mkoa wa Simiyu, ambapo Waziri Mkuu alisisitiza kuwa Serikali ya Awamu ya Sita chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan ipo imara na imejidhatiti kuhakikisha huduma muhimu za kijamii zinawafikia wananchi wote nchini. Katika hotuba yake, Mheshimiwa Majaliwa aliwahakikishia wananchi kuwa Serikali itaendelea kufanya kazi …

Soma zaidi »

UJENZI WA MIUNDOMBINU YA MWENDOKASI AWAMU YA NNE WAENDELEA KWA KASI

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kutekeleza mradi mkubwa wa ujenzi wa miundombinu ya Mabasi Yaendayo Haraka (BRT) awamu ya nne, ikiwa ni juhudi za kuboresha usafiri wa umma jijini Dar es Salaam. Awamu hii inahusisha ujenzi wa njia kuu ya mwendokasi yenye urefu wa kilometa 13.5, inayotoka …

Soma zaidi »

Ijumaa, Desemba 20, 2024, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amekabidhi rasmi nyumba 109 kwa waathirika wa maafa ya maporomoko ya tope yaliyotokea Disemba mwaka jana wilayani Hanang, mkoani Manyara. Nyumba hizo zimejengwa katika kitongoji cha Waret, Hanang, ikiwa ni juhudi za Serikali kurejesha hali ya kawaida kwa waathirika na kuimarisha ustawi wao

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo, Waziri Mkuu amesema kuwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan anawapa pole waathirika wote na kusisitiza dhamira ya Serikali ya kuendelea kuwasaidia. “Ujenzi huu ni ishara ya upendo na kujali kwa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia, aliyetoa maelekezo ya kujenga nyumba bora na za kudumu kwa …

Soma zaidi »

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amefanya mazungumzo na Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Somalia Mheshimiwa Dkt. Hassan Sheikh Mohamud kufuatia mwaliko wa Rais huyo yaliyofanyika katika Ikulu ya Nchi hiyo jijini Mogandishu

Viongozi hao wameelezea kuhusu dhamira yao ya kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na uchumi kati ya mataifa hayo mawili. Waziri Kombo yupo nchini Somalia kwa ziara ya kikazi ambapo aliongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye hafla ya kutia saini hati ya Makubaliano ya Ushirikiano na Jamhuri ya …

Soma zaidi »

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Desemba 19, 2024 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye kuaga mwili wa marehemu John Billy Tendwa ambaye aliwahi kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini.

Akitoa Salama pole kwa waombolezaji wakati wa tukio la kuaga lililofanyika katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia ametoa wito kwa wanafamilia, ndugu na waombolezaji kuyaenzi mema yote aliyoyafanya marehemu Tendwa katika kipindi cha uhai wake. Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Marehemu Tendwa …

Soma zaidi »