Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Mhe. Mhandisi Hamad Yussuf Massauni amesema mpaka sasa jumla ya Miradi 82 ya Biashara ya Kaboni ipo kwenye rejesta na kati ya hiyo, Miradi 4 imeshafika kwenye hatua ya utekelezaji kamili ambapo utasaidia kuiwezesha nchi kupata mapato na kuimarisha ustawi wa wananchi.

Amesema hayo Dodoma Januari 19, 2025 wakati akiwasilisha taarifa kuhusu muundo na majukumu ya Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC) kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira akieleza Biashara ya Kaboni inaendelea kutekelezwa katika Halmashauri mbalimbali zikiwemo Halimashauri za Wilaya za Tanganyika, Kiteto, Karagwe, Uvinza na Mbulu ambapo mwenyekiti wa kamati hiyo ni Mhe. Jackson Kiswaga.

Biashara ya Kaboni ni mfumo wa kiuchumi unaoruhusu uuzaji na ununuzi wa Viwango vya Kaboni. Lengo lake ni kupunguza gesijoto (Green House Gases) angani. Mradi wa Kaboni maana yake ni mradi wowote unaotekelezwa kwa ajili ya kuzalisha Viwango vya Kaboni (Carbon credits) vinavyotambulika kimataifa.

Miongozi mwa faida zinazotokana na Biashara ya Kaboni ni kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na uhifadhi wa Mazingira, kuimarisha Uchumi, Maisha ya Jamii, Sera, Teknolojia na Ubunifu.

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *