Prof. Shemdoe ametoa wito huo kwa uongozi wa Manispaa ya Morogoro, mara baada ya baada ya kumaliza ukaguzi wa ujenzi wa mradi wa Stendi ya Mabasi Madogo Kihonda, stendi ambayo inajengwa karibu na Stesheni ya SGR ya Jakaya Kikwete Morogoro.

“Kuna watu wanatoka mbali wanakuja Stesheni ya Jakaya Kikwete ili waende Dar es Salaam na kurudi jioni lakini wakifika hapo stesheni wanakuta maegesho ya magari yamejaa, hivyo manispaa jengeni maegesho ya magari ambayo yatawaingizia kipato,” ameelekeza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe aitaka Manispaa hiyo ya Morogoro kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ili kurahisisha mchakato wa ujenzi wa magesho ya magari ambayo yatakuwa ni chanzo kipya cha mapato ndani ya mkoa wa Morogoro.

“Ombeni eneo litakalowawezesha kujenga maegesho ya magari, mimi nina watu wengi kwenye magrupu ya WhatsApp wanalalamika kukosa sehemu ya kupaki magari yao pindi wanapotaka kusafiri na treni ya mwendokasi (SGR),” amesisitiza Prof. Shemdoe.
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+