
Amesema hayo Dodoma Januari 19, 2025 wakati akiwasilisha taarifa kuhusu muundo na majukumu ya Kituo cha Taifa cha Kuratibu Kaboni (NCMC) kwa Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Maji na Mazingira akieleza Biashara ya Kaboni inaendelea kutekelezwa katika Halmashauri mbalimbali zikiwemo Halimashauri za Wilaya za Tanganyika, Kiteto, Karagwe, Uvinza na Mbulu ambapo mwenyekiti wa kamati hiyo ni Mhe. Jackson Kiswaga.

Biashara ya Kaboni ni mfumo wa kiuchumi unaoruhusu uuzaji na ununuzi wa Viwango vya Kaboni. Lengo lake ni kupunguza gesijoto (Green House Gases) angani. Mradi wa Kaboni maana yake ni mradi wowote unaotekelezwa kwa ajili ya kuzalisha Viwango vya Kaboni (Carbon credits) vinavyotambulika kimataifa.
Miongozi mwa faida zinazotokana na Biashara ya Kaboni ni kupunguza athari za mabadiliko ya tabianchi pamoja na uhifadhi wa Mazingira, kuimarisha Uchumi, Maisha ya Jamii, Sera, Teknolojia na Ubunifu.
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+