Tangu uhuru mwaka 1963, sekta ya nishati imekuwa mojawapo ya vichocheo vikubwa vya maendeleo ya Tanzania. Awali, nchi ilitegemea kuni, mkaa, na mafuta ya taa kama vyanzo vikuu vya nishati. Hata hivyo, hatua muhimu zimechukuliwa kufanikisha maendeleo ya sekta hii:
1. 1963-1980,Serikali ilianza uwekezaji katika miradi ya umeme wa maji, ikijumuisha Bwawa la Kidatu na Kihansi, kuboresha upatikanaji wa nishati kwa matumizi ya viwanda na wananchi. Shirika la TANESCO lilianza kusimamia ugavi wa umeme.
2. 1980-2000, Kufikia miaka ya 1990, kulikuwa na juhudi za kugundua gesi asilia, ambapo utafiti ulisababisha ugunduzi wa gesi Songosongo na Mnazi Bay. Serikali ilianzisha sera za kuvutia wawekezaji binafsi kwenye sekta ya nishati.
3. 2000-2015, Gesi asilia ilianza kutumika kwa ajili ya kuzalisha umeme na sekta ya viwanda. Miradi mikubwa kama Bomba la Gesi kutoka Mtwara hadi Dar es Salaam ilijengwa. Aidha, mpango wa “Umeme Vijijini” (REA) ulianza, ukilenga kuongeza upatikanaji wa nishati vijijini.
4. 2015-2025, Uongozi wa Rais John Magufuli na Rais Samia Suluhu Hassan ulizingatia miradi mikubwa ya kimkakati kama Mradi wa Umeme wa Maji wa Julius Nyerere (2,115 MW), kuimarisha upatikanaji wa nishati endelevu. Pia, sekta ya nishati jadidifu (upepo na jua) imeanza kushika kasi, sambamba na jitihada za kupunguza utegemezi wa mafuta.
Tangu 1963 hadi 2025, Tanzania imepiga hatua kubwa katika kuhakikisha upatikanaji wa nishati kwa ajili ya maendeleo ya viwanda, biashara, na kuboresha maisha ya wananchi.
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+