Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa (OWM–TAMISEMI) Mhe. Prof. Riziki Shemdoe ameitaka Manispaa ya Morogoro kuona uwezekano wa kujenga sehemu maegesho ya magari pembezoni mwa Mradi wa Stendi ya Mabasi Madogo ya Kihonda inayojengwa kupitia mradi wa TACTIC, ili maegesho hayo yawe ni chanzo kipya cha mapato ya manispaa hiyo.

Prof. Shemdoe ametoa wito huo kwa uongozi wa Manispaa ya Morogoro, mara baada ya baada ya kumaliza ukaguzi wa ujenzi wa mradi wa Stendi ya Mabasi Madogo Kihonda, stendi ambayo inajengwa karibu na Stesheni ya SGR ya Jakaya Kikwete Morogoro.

“Kuna watu wanatoka mbali wanakuja Stesheni ya Jakaya Kikwete ili waende Dar es Salaam na kurudi jioni lakini wakifika hapo stesheni wanakuta maegesho ya magari yamejaa, hivyo manispaa jengeni maegesho ya magari ambayo yatawaingizia kipato,” ameelekeza Prof. Shemdoe.

Prof. Shemdoe aitaka Manispaa hiyo ya Morogoro kushirikiana na Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Morogoro ili kurahisisha mchakato wa ujenzi wa magesho ya magari ambayo yatakuwa ni chanzo kipya cha mapato ndani ya mkoa wa Morogoro.

“Ombeni eneo litakalowawezesha kujenga maegesho ya magari, mimi nina watu wengi kwenye magrupu ya WhatsApp wanalalamika kukosa sehemu ya kupaki magari yao pindi wanapotaka kusafiri na treni ya mwendokasi (SGR),” amesisitiza Prof. Shemdoe.

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *