Mgeni rasmi, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, ameongoza sherehe ya kufunga rasmi Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA), yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, Sabasaba – Barabara ya Kilwa.
Katika hotuba yake, Waziri Mkuu amesisitiza umuhimu wa maonesho haya katika kukuza biashara za ndani, kuvutia wawekezaji, na kuinua uchumi wa taifa kupitia sekta binafsi na ya umma. Pia ametembelea mabanda mbalimbali na kushuhudia ubunifu, bidhaa na huduma zinazozalishwa na Watanzania.
Tazama video hii ujionee namna Tanzania inavyoendelea kusonga mbele kiuchumi kupitia ushiriki wa taasisi, makampuni, na wananchi katika maonesho haya ya kimataifa.
🔔 Usisahau kusubscribe ili kupata taarifa na matukio mengine muhimu ya kitaifa.
#Sabasaba2025 #MaoneshoYaBiashara #WaziriMkuu #TanzaniaInajenga #WekezaneniTanzania
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+