RAIS DKT. SAMIA AMWAGA NEEMA KWA WAVUVI MKOANI TANGA, BOTI ZA KISASA 35 ZA GAWIWA KWA WANANCHI

Tarehe 26.02.2025

Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan akiendelea na ziara yake ya kikazi Mkoani Tanga amegawa boti 35 zenye thamani ya shilingi bilioni 4.47 kwa wavuvi wa Wilaya ya Pangani ikiwa ni awamu ya pili kwa Rais Mhe. Dkt. Samia kutoa boti kwa wavuvi Mkoani Tanga.

Boti hizo zina uwezo wa kubeba mzigo wa samaki wenye tani 3 hadi 4 na zimetoa fursa kwa vijana kujiajiri na kuweza kujipatia vipato vya kujikimu.

Pia, Ugawaji wa boti hizo unaenda sambamba na utoaji wa mikopo isiyokuwa riba kwa wavuvi ili kuwawezesha kuziendesha boti kwa tija na kukuza mitaji yao.

@samia_suluhu_hassan @ikulu_mawasiliano #sisinitanzania #tanzaniayetu #tanga #tanzania #sisinitanzaniampya #maendeleo #DktSamianaTanga

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *