Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imemteua Mhe. Mhe. Majalio Paul Kyara kugombea Kiti cha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Mhe. Satia Mussa Bebwa kugombea Kiti cha Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha Sauti ya Umma (SAU)
Hafla hiyo ya uteuzi iliyofanyika kwenye Ofisi za Tume zilizopo Njedengwa, jijini Dodoma tarehe 27 Agosti, 2025 imeongozwa na Mwenyekiti wa Tume, Mhe. Jaji wa Mahakama ya Rufaa, Jacobs Mwambegele.