Bi. Scolastica Ernest Lole ni miongoni mwa wananchi walioguswa moja kwa moja na fursa za ajira kupitia mradi wa uchimbaji wa madini ya urani unaoendeshwa na Kampuni ya Mantra Tanzania Ltd. Akiwa mfanyakazi wa Ako Group Ltd kampuni iliyopewa zabuni ya kutoa huduma ya chakula, usafi wa mazingira na malazi ya wafanyakazi wa mradi huo, Scolastica anasema maisha yake yamebadilika kwa kiasi kikubwa.
Anasema kuwa kupitia mkataba wa Ako Group na Mantra, watu wengi kutoka vijiji vinavyozunguka mradi wamepata ajira za kudumu na za mkataba, hatua iliyosaidia kupunguza ukosefu wa ajira na kuongeza kipato kwa familia nyingi. Huduma wanazozitoa si tu zinawawezesha kiuchumi, bali pia zimejenga uzoefu wa kazi na taaluma mpya miongoni mwao.
Scolastica anaeleza kwa furaha kuwa uwepo wa mradi huu umekuwa baraka kwa wakazi wa Songea, kwani mbali na ajira, jamii imenufaika na huduma za kijamii kama maji, afya, na miundombinu bora. Anaamini kuwa huu ni mwanzo wa mabadiliko chanya ya kiuchumi kwa mikoa ya kusini na taifa kwa ujumla.
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+