Recent Posts

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Rais wa Umoja wa Mabunge Duniani (IPU), Mhe. Dkt. Tulia Ackson, amefungua na kushiriki hafla ya kumbukizi ya miaka mitano ya Women’s Health Talk Event iliyofanyika katika Hoteli ya Hyatt Regency Mkoani Dar es Salaam

Pamoja na mambo mengine, Dkt. Tulia amewasisitiza washiriki wa hafla hiyo kushiriki katika Uchaguzi wa Serikali za mitaa unaotarajiwa kufanyika Novemba 27, 2024 ili kupata Viongozi sahihi kwa maslahi ya taifa.

Soma zaidi »

Serikali ya Tanzania imewekeza katika miradi mbalimbali ya maji kwa lengo la kufikia upatikanaji wa maji safi na salama kwa asilimia 100 ifikapo mwaka 2030. Hii hapa ni baadhi ya miradi muhimu iliyotekelezwa hadi sasa pamoja na madhumuni na mafanikio yake

Mradi wa Maji wa Ziwa Victoria: Mradi huu unalenga kusambaza maji kutoka Ziwa Victoria hadi mikoa ya Shinyanga, Tabora, na Singida. Umechangia kwa kiasi kikubwa kuongeza upatikanaji wa maji katika maeneo ya mijini na vijijini, ukiwa na uwezo wa kuhudumia maelfu ya wakazi ambao hapo awali walikosa huduma hii muhimu. …

Soma zaidi »

Tanzania Kuandaa Mkutano wa Kilele wa Nishati Januari 2025

Mkutano wa kilele kuhusu nishati unaotarajiwa kufanyika jijini Dar es Salaam mwishoni mwa Januari 2025, ambao unawalenga Wakuu wa Nchi za Kusini mwa Jangwa la Sahara, una umuhimu mkubwa kimkakati kwa maendeleo ya Tanzania na Afrika kwa ujumla. Huu ni mkutano wa kimkakati unaoweza kutoa faida kubwa kwa Tanzania katika …

Soma zaidi »