Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Ajira na Mahusiano, Deus Sangu amewataka wamiliki wa viwanda nchini kuzingatia masuala ya usalama na afya mahali pa kazi ili kulinda ustawi wa wafanyakazi na kuongeza tija ya uzalishaji.

Waziri Sangu ametoa wito huo (Januari 05, 2026) mkoani Mwanza, wakati wa ziara yake maalum ya kukagua utekelezaji wa masuala ya  Usalama na Afya Mahali Pa Kazi katika Kiwanda cha Omega Fish Limited.

Akiwa kiwandani hapo Waziri Sangu amepongeza menejimenti ya kiwanda hicho kwa kutoa ajira kwa wazawa na kuzingatia kwa vitendo sheria, kanuni na taratibu za usalama na afya mahali pa kazi.

Sambamba na hayo, Sangu amevitaka viwanda vyote nchini kushirikiana kwa karibu na Wakala wa Usalama na Afya Mahala Pa Kazi (OSHA) ili kuhakikisha mazingira ya kazi yanakuwa salama, yenye tija na yanayochangia ukuaji wa uchumi wa taifa.  

Awali akizungumza Mkurugenzi Mkuu OSHA, Khadija Mwenda alisema OSHA itaendelea kusimamia wamiliki wa viwanda nchini kutekeleza sheria ya usalama mahala pa kazi katika ili kuwawezesha wafanyakazi na waajiri kutumia muda mwingi katika shughuli za uzalishaji wenye tija.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Kiwanda cha Omega Fish Market Hamad Alsalman ameishukuru Serikali na kuahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa serikali katika kutekeleza majukumu ya kuhakikisha usalama mahala pa kazi  unazingatiwa kisheria.

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *