UKUAJI KATIKA SEKTA YA UTALII

Tanzania imefanikiwa kufanikisha ukuaji mkubwa katika sekta ya utalii wa ndani kati ya mwaka 2021 na 2024, ikivunja rekodi za awali. Mafanikio haya yanatokana na juhudi thabiti na uongozi makini wa Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan, ambaye amekuwa mstari wa mbele katika kuhamasisha utalii wa ndani kupitia kampeni mbalimbali za kimkakati.

Moja ya juhudi kubwa za Mheshimiwa Rais ni uzinduzi wa filamu maarufu ya Royal Tour mwaka 2022, ambayo ilionyesha uzuri wa vivutio vya asili na kiutamaduni vya Tanzania kwa ulimwengu. Filamu hiyo ilifanikiwa si tu kuvutia watalii wa kimataifa, bali pia kuhamasisha Watanzania wengi kutembelea vivutio vyao vya ndani.

#Sisinitanzania #nchiyangukwanza #matokeochanya #kaziiendelee #kazinaututunasongambele #katibanasheria #mslac #SSH

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *