OFISI YA WAZIRI MKUU SERA, BUNGE, KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU

MAENDELEO YANAKUJA KWA KUFANYA KAZI – DKT. BITEKO

“Tangu kuanza kwa mradi wa EACOP mwaka 2022 hadi sasa, jumla ya Watanzania 9,194 wamepata nafasi za kufanya kazi ndani ya mradi na hivyo kuwa fursa kwao ya kujipatia kipato, mwaka 2024 kampuni ilitoa mafunzo maalumu kwa Vijana 170 na kuwapatia kazi kwenye mradi, Vijana wengine 110 wapo katika masomo …

Soma zaidi »

SHEREHE ZA UFUNGAJI RASMI WA MAONESHO YA 49 SABASABA | WAZIRI MKUU KASSIM MAJALIWA

Mgeni rasmi, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa, ameongoza sherehe ya kufunga rasmi Maonesho ya 49 ya Biashara ya Kimataifa ya Dar es Salaam (SABASABA), yaliyofanyika kwenye viwanja vya Mwalimu Nyerere, Sabasaba – Barabara ya Kilwa. Katika hotuba yake, Waziri Mkuu amesisitiza umuhimu wa maonesho …

Soma zaidi »

MRADI WA URANI WALETA AJIRA NA MATUMAINI KWA WAKAZI WA SONGEA SCOLASTICA

Bi. Scolastica Ernest Lole ni miongoni mwa wananchi walioguswa moja kwa moja na fursa za ajira kupitia mradi wa uchimbaji wa madini ya urani unaoendeshwa na Kampuni ya Mantra Tanzania Ltd. Akiwa mfanyakazi wa Ako Group Ltd kampuni iliyopewa zabuni ya kutoa huduma ya chakula, usafi wa mazingira na malazi …

Soma zaidi »

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiongoza Kikao cha Baraza la Mawaziri kilichofanyika Ikulu Chamwino mkoani Dodoma tarehe 14 Julai, 2025. Kikao hicho cha Baraza la Mawaziri ni cha mwisho cha Serikali ya Awamu ya Sita kabla ya kufanyika Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba 2025

Soma zaidi »

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameiagiza Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade) kuendeleza juhudi za kutafuta masoko ya nje ili kuongeza mauzo yatakayowezesha nchi kupata fedha za Kigeni.

Amesema kuwa TanTrade inapaswa kufanya tafiti za uhakika na uchambuzi wa masoko ambayo bidhaa za Tanzania zinaweza kuuzwa na kutoa taarifa hizo kwa wafanyabiashara kote nchini. Ametoa agizo hilo (Jumapili, Julai 13, 2025) alipomwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ufungaji wa Maonesho ya 49 ya Kimataifa ya Biashara ya …

Soma zaidi »

MAJALIWA AMWAKILISHA RAIS DKT. SAMIA IBADA YA KUWEKWA WAKFU ASKOFU MTEULE DKT. DANIEL MONO

WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa leo Julai 13, 2025 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika ibada ya kumweka wakfu na kumuingiza kazini Askofu Mteule Dkt. Daniel Henry Mono wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania, Dayosisi ya Mwanga. Ibada hiyo imefanyika katika kanisa la KKKT Dayosisi ya Mwanga mkoani Kilimanjaro.

Soma zaidi »

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema Tanzania ina umeme wa kutosha hatua ambayo imechangiwa na kukamilika kwa Miradi mikubwa ya uzalishaji umeme ukiwemo Mradi wa Bwawa la Julius Nyerere (JNHPP) ambao pekee unazalisha Megawati 2115

Naibu Waziri Mkuu ameyasema hayo Julai 10, 2025 wakati wa ziara yake ya kukagua maendeleo ya miradi ya kuzalisha umeme kwa gesi asilia katika vituo vya Kinyerezi I, Kinyerezi I Extension na Kinyerezi II ambapo amesema licha ya kazi kubwa inayofanywa na TANESCO yapo baadhi ya maeneo yalikua na changamoto …

Soma zaidi »

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa amesema kuwa Serikali itaendelea kuimarisha mazingira ya ufanyaji biashara za huduma za kifedha ili kuvutia uwekezaji wa ndani na nje kwa kuwa maendeleo endelevu ya taifa hayawezi kufikiwa bila ushiriki thabiti wa sekta binafsi

Amesema kuwa sekta ya fedha ni kichocheo kikubwa katika ukuaji wa Uchumi na ustawi wa wananchi kwa ujumla na ni moja ya sababu inyowezesha maendeleo ya Taifa kwenda kwa kasi. Amesema hayo leo Alhamisi (Julai 03, 2025) wakati wa uzinduzi wa Benki ya Maendeleo PLC, kuwa Benki kamili ya kibiashara, …

Soma zaidi »

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amesema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan anapenda kufanya kazi na viongozi wa dini kwa kuwa anawaongoza wananchi wenye dini ambao dini zao wanaziheshimu na hivyo asingependa kuona haki zao zinanyimwa kwa namna yoyote ile

Dkt. Biteko amesema hayo Julai 3, 2025 jijini Dodoma wakati akimwakilisha Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano Mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT). “Mheshimiwa Rais Samia anapenda kufanya kazi na viongozi wa dini na ninyi ni mashahidi amekuwa akiwaalika ili tuzungumze masuala mbalimbali ya kitaifa …

Soma zaidi »