Benki Kuu ya Tanzania (BoT) imetunukiwa Tuzo Kuu ya Ubunifu katika Huduma Jumuishi za Fedha (Nestor Espenilla Jr. Financial Inclusion Innovation Award) inayotolewa na Jumuiya ya Huduma Jumuishi za Fedha (AFI), yenye wanachama 84 duniani.

Tuzo hiyo ilipokelewa na Naibu Gavana wa BoT anayeshughulikia Uthabiti na Usimamizi wa Sekta ya Fedha, Bi. Sauda Msemo, kwa niaba ya Gavana Bw. Emmanuel Tutuba, katika Mkutano Mkuu wa AFI uliofanyika hivi karibuni mjini Swakopmund, Namibia.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Septemba 15, 2025 wakati akitangaza tuzo hiyo, Mkurugenzi wa Mifumo ya Malipo ya Taifa, Lucy Shaidi, amesema ushindi huo umetokana na ubunifu wa mifumo ya malipo ikiwemo TIPS (Tanzania Instant Payment System) na TANQR (QR Code ya kitaifa ya malipo).

“Mfumo wa TIPS umesaidia kupunguza gharama za miamala kwa wananchi, huku TANQR ukiwarahisishia wafanyabiashara kupokea malipo kupitia benki na kampuni za simu. Ubunifu huu umevutia hata mataifa jirani,” amesema Lucy.

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *