Tuzo hiyo ilipokelewa na Naibu Gavana wa BoT anayeshughulikia Uthabiti na Usimamizi wa Sekta ya Fedha, Bi. Sauda Msemo, kwa niaba ya Gavana Bw. Emmanuel Tutuba, katika Mkutano Mkuu wa AFI uliofanyika hivi karibuni mjini Swakopmund, Namibia.

Akizungumza jijini Dar es Salaam leo Septemba 15, 2025 wakati akitangaza tuzo hiyo, Mkurugenzi wa Mifumo ya Malipo ya Taifa, Lucy Shaidi, amesema ushindi huo umetokana na ubunifu wa mifumo ya malipo ikiwemo TIPS (Tanzania Instant Payment System) na TANQR (QR Code ya kitaifa ya malipo).
“Mfumo wa TIPS umesaidia kupunguza gharama za miamala kwa wananchi, huku TANQR ukiwarahisishia wafanyabiashara kupokea malipo kupitia benki na kampuni za simu. Ubunifu huu umevutia hata mataifa jirani,” amesema Lucy.
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+