Maktaba ya Mwaka: 2024

Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki Mhe. Balozi Mahmoud Thabit Kombo (Mb.) amefanya mazungumzo na Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Somalia Mheshimiwa Dkt. Hassan Sheikh Mohamud kufuatia mwaliko wa Rais huyo yaliyofanyika katika Ikulu ya Nchi hiyo jijini Mogandishu

Viongozi hao wameelezea kuhusu dhamira yao ya kuendelea kuimarisha ushirikiano wa kidiplomasia na uchumi kati ya mataifa hayo mawili. Waziri Kombo yupo nchini Somalia kwa ziara ya kikazi ambapo aliongoza ujumbe wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwenye hafla ya kutia saini hati ya Makubaliano ya Ushirikiano na Jamhuri ya …

Soma zaidi »

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa leo Desemba 19, 2024 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan kwenye kuaga mwili wa marehemu John Billy Tendwa ambaye aliwahi kuwa Msajili wa Vyama vya Siasa nchini.

Akitoa Salama pole kwa waombolezaji wakati wa tukio la kuaga lililofanyika katika Viwanja vya Karimjee Jijini Dar es Salaam, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Rais Dkt. Samia ametoa wito kwa wanafamilia, ndugu na waombolezaji kuyaenzi mema yote aliyoyafanya marehemu Tendwa katika kipindi cha uhai wake. Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa Marehemu Tendwa …

Soma zaidi »

TANZANIA NA OMANI ZASAINI MKATABA WA KUTOTOZA KODI MARA MBILI

Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Kisultan ya Oman, zimetia saini Mkataba wa Kuondoa Utozaji Kodi ya Mapato Mara Mbili na Kuzuia Ukwepaji Kodi, ujulikanao kama Agreement for the Elimination of Double Taxation with Respect to Taxes on Income and Prevention of Tax Avoidance and Evasion. …

Soma zaidi »

Wataalamu wa Ununuzi na Ugavi wametakiwa kutekeleza majukumu yao kwa uadilifu na kufanya kazi kwa kuzingatia sheria, kanuni na miongozo mbalimbali inayosimamia kada ya Ununuzi na Ugavi nchini.

Mhe. Dkt. Biteko alisema kuwa Sekta ya Ununuzi na Ugavi ndio eneo pekee linalochukua takribani asilimia 70 ya Bajeti ya Serikali, hivyo uadilifu pekee ndio utakaosaidia fedha kutumika kwa malengo yaliyokusudiwa hasa katika kutekeleza miradi mbalimbali ya maendeleo inayotekelezwa na Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Rais wa Jamhuri …

Soma zaidi »

Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Mhandisi Hamad Yusuf Masauni awasili katika Ofisi ndogo ya Ofisi ya Makamu wa Rais jijini Dar es Salaam leo Desemba 16,2024, baada ya kuteuliwa hivi karibuni

Waziri Masauni amepokelewa na Katibu Mkuu Ofisi ya Makamu wa Rais Mhandisi Cyprian Luhemeja na Naibu Katibu Mkuu (Muungano) Ofisi ya Makamu wa Rais Bw. Abdallah Hassan Mitawi.

Soma zaidi »

DKT. NCHEMBA AHIMIZA USHIRIKIANO WA KIKODI NA OMAN

Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), akizungumza katika kikao kifupi na Mwenyekiti wa Mamlaka ya Mapato ya Oman, Bw. Nasser Khamis Al-Jashmir, kuhusu namna ya kuimarisha ushirikiano kati ya Oman na Tanzania katika eneo la kodi ili kurahisisha ufanyaji biashara kwa faida ya nchi hizo mbili. …

Soma zaidi »

Rais Mstaafu Dkt. Jakaya Kikwete, ambaye pia ni Mwenyekiti wa Taasisi ya Ubia wa Wadau wa Maji Kusini mwa Afrika (Global Water Partnership (Southern Africa & GWP Africa Coordination Unit), alishiriki Mkutano wa Bodi wa Taasisi hiyo uliofanyika tarehe 13 Desemba, 2024, mjini Pretoria, Afrika Kusini

Miongoni mwa masuala mengine, mkutano huo wa mwisho wa mwaka ulijadili jinsi GWPSA inaweza kuongeza ufanisi na kupanua zaidi shughuli zake za kutoa msaada wa kifedha na kitaalamu katika sekta ya maji kwa nchi nyingi zaidi barani Afrika. Kama sehemu ya mikakati ya kufikia lengo hilo, GWPSA imepanga kushirikiana kwa …

Soma zaidi »

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa leo Desemba 14, 2024 ametembelea kiwanda cha kutengeneza dawa za binadamu cha CURE AFYA kilichopo Kigamboni jijini Dar es Salaam

Akizungumza baada ya kushuhudia uzalishaji wa dawa kwenye kiwanda hicho chenye thamani ya takribani shilingi bilioni 50, Waziri Mkuu amesema kuwa Serikali inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan itaendelea kuweka mazingira rafiki ya uwekezaji ili kuhakikisha wawekezaji wanapata faida kutokana na shughuli zao. “Serikali imefanya uwekezaji mkubwa kwenye …

Soma zaidi »

DKT NCHEMBA AIPA KONGOLE SADC KUTAKA KUANZISHA MFUKO WAKE WA MAENDELEO YA KIUCHUMI

Katibu Mkuu Wizara ya Fedha, Dkt. Natu El-maamry Mwamba, amemwakilisha Waziri wa Fedha, Mhe. Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu (Mb), kushiriki Mkutano wa Dharura wa Kamati ya Mawaziri wa Fedha na Uwekezaji wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC), uliofanyika kwa njia ya mtandao wa Zoom, akiwa katika Ofisi …

Soma zaidi »

Serikali kupitia Ofisi ya Makamu wa Rais imesema itaendeleakushirikiana na Nchi Wanachama wa Jumuiya ya MaendeleoKusini mwa Afrika (SADC) katika kukabiliana na athari zamabadiliko ya tabianchi katika ukanda huo

Hayo yameelezwa Desemba 11, 2024 Jijini Dodoma na NaibuKatibu Mkuu (Mazingira) Ofisi ya Makamu wa Rais, Bi Christina Mndeme wakati wa mazungumzo baina yake naUjumbe wa Wizara ya Maliasili na Mabadiliko ya Tabianchiwa Serikali ya Jamhuri ya Malawi ulioongozwa naMkurugenzi wa Mazingira wa Wizara hiyo, Bi. TawongaMbale-Luka. Mndeme amesema mataifa …

Soma zaidi »