Mkurugenzi wa Ofisi ya Zanzibar ya Tume Huru ya Taifa ya Uchaguzi, Ndg. Adam Mkina leo tarehe 24 Februari, 2026, ametembelea mafunzo kwa Wasimamizi na Wasimamizi Wasaidizi wa vituo vya kupigia kura katika Kata ya Shiwinga iliyopo Halmashauri ya Wilaya ya Mbozi, Mkoani Songwe ambapo amewataka watendaji hao kufanya kazi kwa weledi

Mkina amewaasa washiriki wazingatie mafunzo waliyoyapata na kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao kwa mujibu wa sheria za uchaguzi ili kufanikisha uchaguzi huo.

Amewasisitiza kuzingatia viapo walivyoapa, kuzingatia ujazaji wa fomu za uchaguzi katika hatua zote za uchaguzi ili kuepuka changamoto zinazoweza kujitokeza na kwamba inapotokea changamoto katika vituo washirikiane kuzitatua ili kufanikisha uchaguzi huo.

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *