Naibu Waziri Ofisi Makamu wa Rais (Muungano na Mazingira) Mhe. Dkt. Festo Dugange amefanya mazungumzo na Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais (Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi ) Mhe.Hamza Hassan Juma wakati wa ziara ya kikazi leo Februari 16, 2026 Zanzibar.

Katika mazungumzo yao viongozi hao wamesisitiza umuhimu wa ushirikiano wa Serikali hizo mbili katika kulinda Muungano.

Naibu Waziri Dkt. Dugange alipongeza kazi kubwa ya maendeleo inayofanywa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) chini ya Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi.

Alisema kuwa kupitia maendeleo hayo yanaimarisha uchumi wa Zanzibar na ndio matunda ya Muungano.

Kwa upande wake Waziri Hamza alitoa rai kwa watendaji kutangaza zaidi fursa za zinazopatikana katika Muungano badala ya changamoto.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na viongozi kutoka Ofisi ya Makamu wa Rais na Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar.

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *