Rais wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amemuapisha Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu mpya wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
Katika hotuba yake, Rais Samia amesema uteuzi huo ulipitia ushindani mkubwa na Dkt. Mwigulu ndiye aliyebeba sifa nyingi zaidi kwenye vigezo vyote vilivyopimwa. Ameeleza kuwa majukumu ya Waziri Mkuu yapo wazi kwenye Katiba, lakini pia amemkabidhi vitabu vya mwongozo vitakavyomsaidia kwenye kusimamia kazi za Serikali na kuwatumikia wananchi.
Tazama tukio kamili la kuapishwa, hotuba ya Rais, pamoja na ujumbe alioutoa kwa Waziri Mkuu mpya kuhusu majukumu yake mbele ya Taifa. Usisahau ku-Subscribe kwa taarifa mpya na matukio muhimu ya kitaifa.
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+