Ujenzi wa Daraja la Magufuli (Kigongo-Busisi) Wafikia Asilimia 90.5, Kukamilika Desemba 2024

Ujenzi wa Daraja la J.P. Magufuli (Kigongo–Busisi) umefikia hatua za mwisho. Hadi Septemba 17, 2024, ujenzi ulikuwa umefikia asilimia 90.5, na sehemu ya mita mbili pekee ilibaki ili kuunganisha daraja lote.

Daraja hili lenye urefu wa kilomita 3.2 linatarajiwa kukamilika ifikapo Desemba 2024. Serikali imeendelea kutoa fedha kwa wakati, ambapo hivi karibuni zilitolewa shilingi bilioni 18 kwa ajili ya kukamilisha ujenzi huo.

Kukamilika kwa daraja hili kutarahisisha usafiri na usafirishaji kati ya mikoa ya Mwanza na Geita, na pia nchi jirani kama Uganda, Rwanda, na Burundi.

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *