SIRI YA MTO USIOISHA, DAWA YA ASILI KUTOKA BARAFU ZA MLIMA KILIMANJARO! KILASIYA WATERFALLS:
Kilasiya ni maporomoko ya maji ya kipekee yaliyopewa jina la Kichaga lenye maana ya “kitu kisichoisha.” Maporomoko haya hayakauki hata wakati wa kiangazi, tofauti na maporomoko mengine manne ya Marangu. Kilasiya ilianzishwa mwaka 1991 na Libori George Mosha, Mkazi wa Marangu, kijiji cha Kyala, mkoani Kilimanjaro, kama mradi wa kutunza …
Soma zaidi »Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwahutubia, Majaji, wageni waalikwa pamoja na wananchi kwa ujumla kwenye Maadhimisho ya Siku ya Sheria nchini ambayo Kitaifa yamefanyika katika viwanja vya Chinangali Jijini Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa kwenye picha ya pamoja na Mkurugenzi Mtendaji na Mwenyekiti wa kampuni ya SC Johnson Family Dkt. Fisk Johnson kutoka Marekani pamoja na Rais Mstaafu wa Awamu ya Nne Dkt. Jakaya Mrisho Kikwete, Ikulu Chamwino, mkoani Dodoma
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akimkabidhi Mkuu wa Mkoa wa Tabora Mhe. Paul Matiku Chacha mfano wa ufunguo wa magari kwa ajili ya huduma ya afya inayotembea (Mobile Clinic) kwa Wilaya ya Sikonge na Uyui yaliyotolewa na Jakaya Kikwete Foundation chini ya ufadhili wa Kampuni ya SC Johnson Family ya Marekani
Matukio mbalimbali ya kuwasili kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Robert Mugabe,Harare nchini Zimbabwe kwa ajili ya kuhudhuria Mkutano wa Wakuu wa nchi wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaofanyika leo tarehe 31 Januari, 2025
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ni Mwenyekiti wa Asasi ya Siasa, Ulinzi na Usalama ya Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC-Organ) Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akishiriki Mkutano wa Dharura wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa SADC katika ukumbi wa New Parliament Building, Harare nchini Zimbabwe tarehe 31 Januari, 2025
Mkutano huo pamoja na mambo mengine unajadili hali ya ulinzi na usalama Mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo (DRC).
Soma zaidi »Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Shirikisho la Jamhuri ya Somalia Mhe. Dkt. Hassan Sheikh Mohamud leo kwenye makazi yake Ikulu, Jijini Dar es salaam leo
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Philip Isdor Mpango akikagua mabanda ya maonesho ya wadau wa sekta ya maji nje ya Ukumbi wa Mikutano wa Mlimani City mkoani Dar es Salaam kabla ya kufungua Kongamano la Nne la Kimataifa la Kisayansi la Maji linalofanyika kwa siku tatu kuanzia Jumatano Januari 29, 2025 mpaka Ijumaa Januari 31, 2025
Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akifanya Mazungumzo na NaibuMkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Fedha la Kimataifa (IMF) Bw. Bo Li
Mazungumzo hayo yalifanyika kando ya Mkutano waNishati wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Afrika unaofanyikakatika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNICC)
Soma zaidi »
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+