DCEA YANASA VIJANA WAKITENGENEZA BISKUTI ZA BHANGI KWA AJILI YA HOUSE PARTY

Katika operesheni maalum iliyofanyika eneo la Mlalakuwa, wilayani Kinondoni jijini Dar es Salaam, Mamlaka ya Kudhibiti na Kuapmbana na Dawa za Kulevya (DCEA) wamewakamata vijana wanne wakidaiwa kutengeneza biskuti za bangi kwa ajili ya sherehe ya wanafunzi wa vyuo vikuu.

Watuhumiwa hao ni Bright A. Malisa (26), Humphrey G. Safari (26), Novatus A. Kileo (26) na Chriss P. Mandoza (26). Wakati wa upekuzi, walikutwa na biskuti 140 za bangi, puli nane na paketi tisa za bangi zenye jumla ya uzito wa kilo 2.858.

Kamishan Jenerali wa DCEA Aretas Lyimo ameeleza kuwa taarifa za awali zinaeleza kuwa vijana hao walikuwa wakijiandaa kusambaza biskuti hizo katika house party iliyopangwa kufanyika mwishoni mwa wiki, ikihusisha wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali jijini Dar es Salaam.

Polisi wamesema uchunguzi zaidi unaendelea ili kubaini mtandao mpana unaohusiana na utengenezaji na usambazaji wa bidhaa hizo za dawa za kulevya.

#KataaDawaZaKulevyaTimizaMalengoYako

Piga 119 kutoa taarifa

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *