
Dkt. Biteko amesema hayo Julai 3, 2025 jijini Dodoma wakati akimwakilisha Rais Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Mkutano Mkuu wa 32 wa Jumuiya ya Kikristo Tanzania (CCT).
“Mheshimiwa Rais Samia anapenda kufanya kazi na viongozi wa dini na ninyi ni mashahidi amekuwa akiwaalika ili tuzungumze masuala mbalimbali ya kitaifa ingekuwa ni mtu anayejifungia ndani na akasema analo jeshi, sheria, katiba na vyombo vya ulinzi basi nitafanya kazi nadhani hivi ingekuwa ngumu sana lakini yeye amesema milango yetu iwe wazi tuzungumze na viongozi wa dini kwa ajili ya kutafuta mustakabali wa nchi yetu pale ambapo tunadhani hatuendi sawasawa,” amesema Dkt. Biteko.

Akijibu hoja za CCT, Dkt. Biteko amesema kuwa imekuwa desturi ya nchi kuwa na waangalizi wa ndani kwenye Uchaguzi Mkuu na kuwa ni imani yake kuwa Tume Huru ya Uchaguzi itawalika waangalizi wa ndani ikiwa ni pamoja na asasi za kiraia. Hata hivyo amesisitiza Tume Huru ya Uchaguzi iachiwe uhuru wake wa kufanya kazi zake.

Amewahakikishia kuwa Serikali inatambua na kuthamini kazi kubwa inayofanywa na taasisi zote za dini ikiwemo makanisa na kusema kuwa tangu Uhuru mwaka 1961, Taasisi za dini zimeendelea kuchangia maendeleo ya kijamii na kiuchumi na kuwanufaisha watu wengi kote nchini.
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+