Shamba La Kahawa La Aviv, Moja Ya Uwekezaji Mkubwa Wa Ukulima Wa Kahawa Nchini.

‘Katika ziara yangu ya kikazi mkoani Ruvuma, leo nimetembelea shamba la Kahawa la Aviv, moja ya uwekezaji mkubwa wa ukulima wa kahawa nchini. Nimeagiza kuendelea kuhakikisha teknolojia inayotumika kwa ufanisi kwenye uwekezaji wa aina hii itumike pia katika kuwapa ujuzi wananchi ili washiriki kikamilifu katika fursa zilizopo.

Mbali na ajira, uwekezaji wa shamba hili unatoa mchango mkubwa katika utunzaji wa Bonde la Mto Ruvuma ambalo ni tegemeo la maisha ya mamilioni ya wananchi katika mikoa ya Ruvuma, Mtwara na Lindi.”

Mhe. Rais. Dkt. Samia Suluhu Hassan

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *