Tanzania

“Tujitokeze Tupige Kura Kwa Viongozi Wanaotamani Kuona Tanzania Ikisonga Mbele”

Tusikubali kusimama pembeni wakati wa uamuzi muhimu. Kwa pamoja, tukiwa na umoja na uzalendo, tujitokeze kwa wingi siku ya kupiga kura, tuweke sauti yetu kwa viongozi wanaotamani kuona Tanzania ikisonga mbele. Tukumbuke kuwa kila kura ina umuhimu na maana kubwa kwa mustakabali wa nchi yetu.

Soma zaidi »

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amesema kuwa matumizi ya mfumo wa kielektroniki wa Baraza la Mawaziri utasaidia kuboresha utendaji kazi na kuleta ufanisi zaidi katika kuwahudumia wananchi

Amesema kuwa maboresho hayo ya matumizi ya mfumo wa kielektroniki yatasaidia kwa kiasi kikubwa kupunguza matumizi ya karatasi katika vikao vya Serikali, hususan Baraza la Mawaziri, hivyo kupunguza changamoto ikiwemo kuchelewa kwa taarifa, gharama kubwa za uchapaji na hatari ya upotevu wa taarifa muhimu. Amesema hayo leo (Jumatatu, Novemba 11, …

Soma zaidi »

TRENI YA MCHONGOKO YAANZA SAFARI KWA KISHINDO DAR – DOM

Treni ya Umeme ya Kisasa (EMU) ya Reli ya Kisasa (SGR) nchini Tanzania ni sehemu muhimu ya mradi wa kuboresha miundombinu ya usafiri wa reli. Treni hizi zina uwezo wa kubeba abiria wengi kwa wakati mmoja na kusafiri kwa kasi ya hadi kilomita 160 kwa saa, hivyo kupunguza muda wa …

Soma zaidi »

Ujenzi wa Daraja la Magufuli (Kigongo-Busisi) Wafikia Asilimia 90.5, Kukamilika Desemba 2024

Ujenzi wa Daraja la J.P. Magufuli (Kigongo–Busisi) umefikia hatua za mwisho. Hadi Septemba 17, 2024, ujenzi ulikuwa umefikia asilimia 90.5, na sehemu ya mita mbili pekee ilibaki ili kuunganisha daraja lote. Daraja hili lenye urefu wa kilomita 3.2 linatarajiwa kukamilika ifikapo Desemba 2024. Serikali imeendelea kutoa fedha kwa wakati, ambapo …

Soma zaidi »

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa amewataka watendaji wote Serikalini wahakikishe vipaumbele vilivyoanishwa kwenye Mpango wa Maendeleo wa Taifa wa Mwaka 2025/2026 vinatafsiriwa vema kwenye mipango ya Taasisi zao

Amesema mpango huo umejikita katika kuendeleza na kukamilisha utekelezaji wa afua zinazotoa matokeo ya maeneo matano ya kipaumbele ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa wa Miaka Mitano. Waziri Mkuu ameyasema hayo leo (Ijumaa, Novemba 8, 2024) wakati akiahirisha Mkutano wa 17 wa Bunge la 12 Bungeni jijini Dodoma, …

Soma zaidi »

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko anaiwakilisha Serikali katika sherehe za uapisho wa Rais Mteule wa Botswana Gideon Duma Boko zitakazofanyika Katika Uwanja wa Taifa wa nchi hiyo Novemba 8, 2024

Akiwasili katika Uwanja wa ndege wa Gaborone, Dkt. Biteko amepokelewa na Katibu Mkuu wa Vijana, Jinsia, Utamaduni na Michezo, Bridget John, Balozi wa Tanzania Nchini Afrika Kusini, Mhe. James Bwana pamoja na maafisa wengine waandamizi wa Nchi hiyo. Mhe. Gideon Duma Boko ni Rais wa Sita Botswana kupitia chama cha …

Soma zaidi »

AMAZING TANZANIA FILM -Rais wa Tz Dkt Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanziba Dkt Hussein Ally Mwinyi

“Amazing Tanzania” ni filamu iliyorekodiwa kwa lugha za Kichana, kiswahili na Kiingereza ambayo Washiriki wakuu ni Rais wa Tanzania Dkt Samia Suluhu Hassan na Rais wa Zanziba Dkt Hussein Ally Mwinyi ambayo inaonyesha uzuri wa Tanzania kupitia mandhari ya kipekee, utamaduni wa kuvutia, na wanyamapori wa ajabu. Filamu hii imeangazia …

Soma zaidi »