MACHINGA MKOANI MOROGORO WASIMAMA NA RAIS KATIKA UJENZI WA TAIFA DHIDI YA WAPINGA MAENDELEO YA NCHI

Wafanyabiashara ndogo ndogo (Machinga) mkoani Morogoro wameonyesha mshikamano wao na Rais Samia Suluhu Hassan katika juhudi za kujenga taifa. Wamejitokeza kwa wingi kuunga mkono miradi ya maendeleo na sera za serikali, wakikemea vikali wale wanaopinga juhudi za kuleta maendeleo nchini. Machinga hao wamesisitiza kuwa wako tayari kushirikiana na serikali katika kuhakikisha nchi inasonga mbele na kukuza uchumi, huku wakieleza kuwa vitendo vya wapinga maendeleo havina nafasi katika Tanzania ya leo. Mkutano huu umeonyesha nia thabiti ya wananchi katika kuunga mkono jitihada za serikali ya awamu ya sita katika kujenga uchumi imara na maendeleo endelevu.

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *