Ina kasi ya hadi kilomita 160 kwa saa kwa treni za abiria na kilomita 120 kwa saa kwa treni za mizigo. Kasi hii inafanya iwezekane kusafirisha abiria na mizigo kwa muda mfupi zaidi ukilinganisha na njia nyingine za usafiri.
Kasi kubwa ya treni za abiria itapunguza muda wa safari kati ya miji mikubwa kama Dar es Salaam na Mwanza, hivyo kuboresha urahisi wa kusafiri na kuongeza shughuli za kibiashara na utalii.
Reli hii itawezesha usafirishaji wa mizigo kwa haraka na kwa gharama nafuu ikilinganishwa na barabara. Hii itasaidia wafanyabiashara kupunguza gharama za usafirishaji na kuongeza faida.
SGR inatarajiwa kuvutia uwekezaji zaidi nchini, kwani miundombinu bora ya usafirishaji ni moja ya vigezo muhimu vinavyohamasisha wawekezaji.
Mradi huu umeunda ajira nyingi kwa Watanzania katika ujenzi na utaendelea kutoa ajira katika uendeshaji na matengenezo ya reli.
Usafirishaji wa haraka na rahisi wa malighafi na bidhaa kumaliza utasaidia viwanda kupata malighafi kwa wakati na kusafirisha bidhaa zao kwa urahisi, hivyo kuchochea ukuaji wa sekta ya viwanda.
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+