Daraja la J.P. Magufuli (Kigongo – Busisi), lenye urefu wa kilomita 3.0 na barabara unganishi ya kilomita 1.66, linatarajiwa kuanza kutumika tarehe 30 Disemba 2024. Daraja hili linalojengwa na kampuni ya China Civil Engineering Construction Corporation na China Railway 15 Bureau Group Corporation (CCECC – CR15G JV) kwa gharama ya Shilingi Bilioni 592.6 bila VAT, linajumuisha njia mbili za magari zenye upana wa meta 7.0 kila upande, njia za maegesho ya dharura meta 2.5, na njia za watembea kwa miguu meta 2.5 kila upande. Ujenzi wa daraja umefikia asilimia 88.61, na utatoa faida kama kupunguza msongamano wa magari, kuimarisha usafiri masaa 24, na kuwa kiungo muhimu kwa Mkoa wa Mwanza na nchi jirani.
Matokeo ChanyA+ Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+. #InfoChanyA+