RAIS WA ZANZIBAR DKT. MWINYI AFANYA MAZUNGUMZO NA WAZIRI WA ULINZI ELIAS KUANDIKWA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amempongeza Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Elias Kuandikwa kwa uteuzi alioupata na kuahidi kuendelea kushirikiana nae.

Rais Dk. Hussein Mwinyi aliyasema hayo leo Ikulu Jijini Zanzibar wakati alipofanya mazungumzo na Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa Elias John Kuandikwa aliyefika Ikulu kwa ajili ya kujitambulisha na kumsalimia Rais ambapo pia, Waziri huyo alifuatana na Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Faraji Mnyepe.

Katika mazungumzo hayo, Rais Dk. Hussein Mwinyi alieleza jinsi alivyofarajika na uteuzi wa Waziri huyo kutokana na uwezo wake mkubwa wa uongozi na kuahidi kumpa mashirikiano makubwa ili iwe ni chachu katika utekelezaji wa kazi zake ndani ya Wizara hiyo.

Rais Dk. Hussein alisema kuwa kwa vile Wizara hiyo ni ya Muungano ana matumaini makubwa kwamba ataendelea kuwa karibu na Waziri huyo katika kuhakikisha anatekeleza vyema majukumu yake sambamba na kuhakikisha Brigedi za Zanzibar zinaendelea kuimarika zaidi.

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *