ALLAN KIJAZI AKABIDHI MAGARI 9 YA MRADI WA KUSIMAMIA MALIASILI NA KUKUZA UTALII KUSINI MWA TANZANIA

Kamishna wa Uhifadhi TANAPA na Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii Dkt. Allan Kijazi jijini Dodoma amekabidhi magari 9 ya Mradi wa Kusimamia Maliasili na Kukuza Utalii Kusini mwa Tanzania unaofadhiliwa na Benki ya Dunia kwa Hifadhi za Mikumi, Ruaha na Udzungwa.

Dkt.Kijazi amesema kuwa magari haya yatatumika kuimarisha na kuboresha shughuli za uhifadhi na utalii katika hifadhi husika.

Kwa upande wake Kamishna Msaidizi Mwandamizi Betrita Lyimo anayesimamia mradi huo kwa upande wa TANAPA
amesema kuwa magari haya ni awamu ya pili ya magari 23 yaliyolengwa kwa ajili ya mradi huo na kusema kuwa magari haya yanatarajiwa kuimarisha shughuli za doria pamoja na kuhudumia watalii.

Naibu Kamishna Steria Ndaga ambaye ni Mkuu wa Kanda ya Mashariki aliahidi kusimamia magari hayo pamoja na mipango mingine yote ili kuhakikisha kuwa lengo la mradi huo kwa ukanda wa kusini linatimizwa kwa wakati na kuleta tija ilihokusudiwa.

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *