MIRADI YA UJENZI WA MAHAKAMA YAENDELEA KWA KASI JIJINI DODOMA

 Na Stanslaus Makendi, Mahakama Kuu Dodoma

Mahakama ya Tanzania inatekeleza miradi mbalimbali ya ukarabati na ujenzi wa Mahakama nchini kwa lengo la kuboresha miundombinu yake ili kuwa na mazingira wezeshi ya utaoji wa huduma ya utoaji haki kwa ujumla.

Ad

Mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa Mikoa kadhaa nchini ambapo miradi mikubwa ya ujenzi wa Mahakama inaendelea. Kwa mwaka wa fedha 2020/2021 Mahakama ya Tanzania inatekeleza jumla ya miradi mitano ya ujenzi wa Mahakama katika Mkoa huo; ikiwemo ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Mahakama, Kituo Jumuishi ya Utoaji haki (Intergrated Justice Centre), Mahakama za Wilaya Chemba na Bahi na Mahakama ya Mwanzo Kibaigwa.

Aidha, hatua ya maboresho ya miundombinu ya majengo ya Mahakama nchini inalenga pia kusogeza huduma za haki karibu zaidi na wananchi ili kumuwezesha mwananchi kupata huduma kwa haraka kwa kupunguza umbali na gharama katika kutafuta huduma ya haki. 

Pichani ni picha za miradi ya ujenzi inayoendelea jijini Dodoma.

Ad

Unaweza kuangalia pia

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuboresha taarifa zake kwenye Daftari la Kudumu la Mpiga Kura, Chamwin

Tarehe 17 Mei, 2025 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *