MIRADI YA UJENZI WA MAHAKAMA YAENDELEA KWA KASI JIJINI DODOMA

 Na Stanslaus Makendi, Mahakama Kuu Dodoma

Mahakama ya Tanzania inatekeleza miradi mbalimbali ya ukarabati na ujenzi wa Mahakama nchini kwa lengo la kuboresha miundombinu yake ili kuwa na mazingira wezeshi ya utaoji wa huduma ya utoaji haki kwa ujumla.

Mkoa wa Dodoma ni miongoni mwa Mikoa kadhaa nchini ambapo miradi mikubwa ya ujenzi wa Mahakama inaendelea. Kwa mwaka wa fedha 2020/2021 Mahakama ya Tanzania inatekeleza jumla ya miradi mitano ya ujenzi wa Mahakama katika Mkoa huo; ikiwemo ujenzi wa jengo la Makao Makuu ya Mahakama, Kituo Jumuishi ya Utoaji haki (Intergrated Justice Centre), Mahakama za Wilaya Chemba na Bahi na Mahakama ya Mwanzo Kibaigwa.

Aidha, hatua ya maboresho ya miundombinu ya majengo ya Mahakama nchini inalenga pia kusogeza huduma za haki karibu zaidi na wananchi ili kumuwezesha mwananchi kupata huduma kwa haraka kwa kupunguza umbali na gharama katika kutafuta huduma ya haki. 

Pichani ni picha za miradi ya ujenzi inayoendelea jijini Dodoma.

Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *