WAZIRI MKUU MAJALIWA AFUNGUA MAONYESHO YA PILI YA TEKINOLOJIA YA DHAHABU MJINI GEITA

GG 1-01
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kuhusu noti bandia na noti halali kutoka kwa Angela Kashanga (kulia) wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) wakati alipotembelea banda la BOT katika Maonyesho ya Tekinolojia ya Dhahabu yaliyofunguliwa na Waziri Mkuu, kwenye uwanja wa CCM Kahangalala mjini Geita, Septemba 22, 2019. Kushoto ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel na katikati ni Mkurugenzi wa BOT tawi la Mwanza, Florence Kazimoto. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)
GG 2-01
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kuhusu noti bandia na noti halali kutoka kwa Angela Kashanga wa Benki Kuu ya Tanzania (BOT) wakati alipotembelea banda la BOT katika Maonyesho ya Tekinolojia ya Dhahabu yaliyofunguliwa na Waziri Mkuu, kwenye uwanja wa CCM Kahangalala mjini Geita, Septemba 22, 2019.
GG 3-01
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akipata maelezo kutoka kwa Mtalaam wa Uchenjuaji madini, John Ngenda ( wa pili kulia) kuhusu mtambo wa kuchenjua madini wakati alipofungua Maonyesho ya Pili ya Tekinolojia ya Dhahabu kwenye uwanja wa CCM, Kahangalala mjini Geita, Septemba 22, 2019. Watatu kulia ni Waziri wa Madini, Doto Biteko na kulia ni Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi Robert Gabriel.
GG 4-01
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akikata utepe kuzindua Mwongozo wa Unaoonyesha Fursa za Uwekezaji wakati alipofungua Maonyesho ya Tekinolojia ya Dhahabu kwenye uwanja wa Kahangalala mjini Geita, Septemba 22, 2019. Wengine pichani kutoka kushoto ni Waziri wa Nishati, Dkt. Medard Kalemani, Waziri wa Madini, Doto Biteko, Mkuu wa Mkoa wa Geita, Mhandisi, Robert Gabriel
GG 5-01
Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akizungumza wakati alipozindua Maonyesho ya Pili ya Tekinolojia ya Dhahabu kwenye uwanja wa CCM Kahangalala mjini Geita, Septemba 22, 2019. (Picha na Ofisi ya Waziri Mkuu)

Unaweza kuangalia pia

UCHUMI WA TANZANIA WAZIDI KUKUA NA KUIMARIKA

Hali ya uchumi wa Tanzania yazidi kuimarika na kukua  kwa asilimia 6.9 ikiwa ni  takwimu …

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *