Matokeo ChanyA+

Chombo kinachounga mkono matokeo yote chanyA+ TanzaniA+.

NAIBU WAZIRI MGALU ALIRIDHISHWA NA MIUNDOMBINU YA UMEME MRADI SGR

Naibu Waziri wa Nishati, Subira Mgalu amesema ameridhishwa na ujenzi wa miundombinu ya njia ya kusafirisha umeme wa kV 220 inayoendelea kujengwa katika Reli ya kisasa kutoka jijini Dar es salaam hadi mkoani Morogoro. Mgalu alieleza hayo Desemba 7,2019 baada ya kufanya ziara ya kukagua maendeleo ujenzi wa miundombinu hiyo …

Soma zaidi »

SERIKALI KUPUNGUZA BEI YA KUUNGANISHA UMEME KATIKA MIJI NA MANISPAA

Naibu Waziri wa Nishati Subira Mgalu amesema Serikali inaaangalia namna ya kufanya tathmini ya kupunguza bei ya kuunganisha umeme kwa wateja waliopo katika Miji na Manispaa ili huduma hiyo iweze kumfikia kila mmoja na kuondoa malalamiko. Mgalu alisema hayo, Desemba 6,2019, baada ya kubaini  changamoto mbalimbali zilizoibuliwa na wawekezaji na …

Soma zaidi »

RAIS DKT. MAGUFULI AWEKA MAWE YA MSINGI MIRADI YA UJENZI WA MELI MPYA YA M.V MWANZA (Hapa Kazi Tu), CHELEZO, PAMOJA NA UKARABATI WA M.V VICTORIA NA M.V BUTIAMA KATIKA ZIWA VICTORIA

Rais Dkt. John Pombe Magufuli tarehe 08 Desemba, 2019 ameweka jiwe la msingi katika miradi ya ujenzi wa meli mpya ya MV Mwanza Hapa Kazi Tu, Chelezo na ukarabati wa meli za MV Victoria na MV Butiama katika Ziwa Victoria. Sherehe za uwekaji jiwe la msingi katika miradi hiyo zimefanyika …

Soma zaidi »

TRA YANG’ARA TUZO ZA NBAA, YAPATA USHINDI WA JUMLA

Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) imeshinda tuzo mbili ikiwemo mshindi wa jumla katika uandaaji bora wa taarifa za hesabu mwaka 2018 kwa kufuata viwango vya Kimataifa vya Uandaaji wa Hesabu katika Taasisi za Umma yaani mfumo wa IPSASs. Katika hafla ya utoaji wa tuzo hizo iliyofanyika katika Kituo cha Mikutano …

Soma zaidi »

EURO MILIONI 140 ZA ACP KUWANUFAISHA WAKULIMA WA MAHINDI NA KOROSHO

Jumla ya Euro milioni 140 zimetengwa ili kuwanufaisha wakulima wa mazao ya korosho na mahindi katika mpango maalum wa kutoa mikopo,kujenga uwezo katika uzalishaji,masoko,uwekezaji na kuongeza mnyororo wa thamani wa mazao hayo kwa wakulima wa nchi za Afrika,Caribbean na Pacific jambo litakalosaidia kupunguza umasikini na njaa katika nchi hizo. Akizungumza …

Soma zaidi »