KENANI AKAGUA MRADI WA MAJI WA BILIONI 520

Mkuu wa Wilaya ya Arusha Kenani Kihongosi amefanya ziara ya kikazi Kukagua mradi wa Maji wa Bilioni 520 akiambatana na Madiwani wa jiji la Arusha wakiongozwa na Mstahiki Meya wa Jiji la Arusha Maximillian Iraghe pamoja na watendaji wa kata katika Jiji la Arusha.

Mkuu wa Wilaya amesema kuwa mradi huo utawanufaisha wananchi na kwa sasa upo hatua nzuri na kusema kuwa Serikali ipo kazini kuhakikisha maendeleo makubwa yanawanaufaisha wananchi.

Mkuu wa Wilaya amewapongeza Mamlaka ya Maji AUWSA na kuwaagiza wakamilishe mradi kwa wakati ili Wananchi waanze kupata maji safi na salama.





Unaweza kuangalia pia

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akiwa na viongozi mbalimbali kwenye picha ya pamoja na baadhi ya Maafisa na Askari wa Kikosi Kazi kutoka Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) walioshiriki Ujenzi wa Makao Makuu ya Ulinzi wa Taifa (MMUT), Kikombo Mkoani Dodoma

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *